LOGO


“Najisikia furaha sana kuwa mshindi”- Mbwana Samatta

“Najisikia furaha sana kuwa mshindi”- Mbwana Samatta

Pia Samata aliwapongeza wachezaji aliowashinda katika mchuano huo na kuwataka wasikate tamaa wazidi kujituma
MSHINDI wa tuzo ya mchezaji bora wa Tanzania kwa mwaka 2014 inayotolewa na Mtandao wa Goal.com Mbwana Samata amewataka wachezaji chipukizi kujitambua ili wapate mafanikio nilazima wajitume na waweke mbele kile ambacho wanakikusidia.
Samata aliyeshinda tuzo hiyo baada ya kuwashinda wanasoka wenzake wanne ambao ni Mrisho Ngasa, Jonas Mkude, Salum Abubakar na Thomas Ulimwengu amesema tuzo hiyo itamuongezea ari ya kuzidi kujituma na kufanya mazoezi kwanguvu ili aweze kushinda tena tuzo hiyo mwaka huu.
“Najisikia furaha sana kuwa mshindi wa tuzo hiyo inayotolewa kwamara ya kwanza Tanzania na Mtandao wenu wa Goal kwani inaonyesha ni kiasi gani mnathamini jitihada zangu na inanipa hamasa yakuzidi kujituma na kuendelea kupokea tuzo hiyo kila mwaka kwani inamuongezea heshima hata kwenye klabu yake anayochezea ya TP Mazembe,”anasema .
Pia Samata aliwapongeza wachezaji aliowashinda katika mchuano huo na kuwataka wasikate tamaa wazidi kujituma kwani licha ya kuibuka na ushindi lakini nao walistahili kuwa washindi kutokana na kuwa na viwango vya juu mwaka 2014, lakini anafurai kuona ameshinda yeye tuzo hiyo.

goal.com

0 comments Blogger 0 Facebook

Chapisha Maoni

ZILIZOSOMWA SANA

 
TASWIRA MICHEZONI © 2015. All Rights Reserved. This Blog Proudly Designed by MMC™ Media Group Ltd | Phone +255-786-758-021
Top