
“Najisikia furaha sana kuwa mshindi”- Mbwana Samatta
Pia Samata aliwapongeza wachezaji aliowashinda katika mchuano huo na kuwataka wasikate tamaa wazidi kujitumaSamata aliyeshinda tuzo hiyo baada ya kuwashinda wanasoka wenzake wanne ambao ni Mrisho Ngasa, Jonas Mkude, Salum Abubakar na Thomas Ulimwengu amesema tuzo hiyo itamuongezea ari ya kuzidi kujituma na kufanya mazoezi kwanguvu ili aweze kushinda tena tuzo hiyo mwaka huu.
“Najisikia furaha sana kuwa mshindi wa tuzo hiyo inayotolewa kwamara ya kwanza Tanzania na Mtandao wenu wa Goal kwani inaonyesha ni kiasi gani mnathamini jitihada zangu na inanipa hamasa yakuzidi kujituma na kuendelea kupokea tuzo hiyo kila mwaka kwani inamuongezea heshima hata kwenye klabu yake anayochezea ya TP Mazembe,”anasema .
Pia Samata aliwapongeza wachezaji aliowashinda katika mchuano huo na kuwataka wasikate tamaa wazidi kujituma kwani licha ya kuibuka na ushindi lakini nao walistahili kuwa washindi kutokana na kuwa na viwango vya juu mwaka 2014, lakini anafurai kuona ameshinda yeye tuzo hiyo.
goal.com
0 comments Blogger 0 Facebook
Chapisha Maoni