LOGO

Jack Warner
Makamu wa Rais wa zamani wa Shirikisho la Kandanda duniani FIFA Jack Warner amekumbwa na kashfa ingine na uchunguzi dhidi yake kuhusiana na kupotea kwa fedha ambazo zililengwa kwa ajili ya kuwasaidia waathirika wa tetemeko la ardhi lililoikumba Haiti mwaka 2010.
Warner aliitembelea nchi hiyo miezi kadhaa baada ya tetemeko hilo a kuchangisha kiasi cha dola dola mia saba na elfu 50 kutoka FIFA na shirika la mpira wa miguu la Korea kusini kwa ajili ya kuijenga upya nchi hiyo.
Lakini hata hivyo, Wachunguzi wa kashfa hiyo rushwa inayoikabili FIFA wanasema fedha hizo zilihamishwa katika Akaunti inayodhibitiwa na Bwana Warner kwa ajili ya matumizi yake binafsi. Miaka minne baadaye fedha hizo bado hazijatolewa maelezo.Warner mwenyewe amekana tuhuma zote zilizotolewa dhidi yake.

0 comments Blogger 0 Facebook

Chapisha Maoni

:) :)) ;(( :-) =)) ;( ;-( :d :-d @-) :p :o :>) (o) [-( :-? (p) :-s (m) 8-) :-t :-b b-( :-# =p~ $-) (b) (f) x-) (k) (h) (c) cheer
Click to see the code!
To insert emoticon you must added at least one space before the code.

ZILIZOSOMWA SANA

 
TASWIRA MICHEZONI © 2015. All Rights Reserved. This Blog Proudly Designed by MMC™ Media Group Ltd | Phone +255-786-758-021
Top