

Jumamosi Septemba 27
Liverpool 1 Everton 1
Chelsea 3 Aston Villa 0
Crystal Palace 2 Leicester 0
Hull 2 Man City 4
Man United 2 West Ham 1
Southampton 2 QPR 1
Sunderland 0 Swansea 0
Vinara wa Ligi Kuu England Chelsea Leo wakicheza kwao Stamford Bridge wameitandika Aston Villa Bao 3-0 na kuzidi kupaa kileleni.
Hadi Mapumziko Chelsea walikuwa mbele kwa Bao 1-0 kwa Bao la Oscar la Dakika ya 7 alilofunga baada ya juhudi binafsi za Willianna Shuti lake kuokolewa na Kipa Brad Guzan lakini Mpira ukamrudia yeye na akampasia Oscar aliefunga.
Dakika ya 59 Diego Costa aliipa Chelsea Bao la Pili kwa Kichwa alipounganisha Krosi ya Cesar Azpilicueta.
Willian aliipa Chelsea Bao la 3 katika Dakika ya 79 baada ya Shuti la Diego Costa kuokolewa na Kipa Guzan na kumkuta Willian.
VIKOSI:
CHELSEA: Courtois, Ivanovic, Azpilicueta, Terry, Cahill, Hazard, Willian, Oscar, Matic, Fàbregas, Diego Costa
Akiba: Cech, Filipe Luis, Zouma, Drogba, Mikel, Schürrle, Remy
ASTON VILLA: Guzan, Hutton, Senderos, Cissokho, Baker, Delph, Cleverley, Westwood, Richardson, Agbonlahor, Weimann
Akiba: Clark, Bacuna, Bent, Sánchez, N'Zogbia, Given, Grealish
REFA: Phil Dowd
CRYSTAL PALACE 2 LEICESTER CITY 0
BAO za Kipindi cha Pili za Fraizer Campbell, Dakika ya 51, na Mile Jedinak, Dakika ya 54, zimewapa ushindi wa Bao 2-0 Crystal Palace waliokuwa Nyumbani wakicheza na Leicester City.
VIKOSI:
CRYSTAL PALACE: Mignolet
Akiba:
LEICESTER CITY: Howard,
Akiba:
REFA: Keith Stroud
HULL CITY 2 MAN CITY 4
Hull City wakicheza kwao na Mabingwa Watetezi Man City walichapwa Bao 4-2 licha ya kujitutumua kutoka 2-0 nyuma na kusawazisha Bao hizo zote.
Kipindi cha Kwanza Man City walikuwa mbele kwa Bao 2-0 ndani ya Dakika 11 za kwanza kwa Bao za Srgio Aguero, Dakika ya 7, Edin Dzeko, Dakika ya 11, lakini Beki wao Eliaquim Mangala alikuwa majanga baada ya kujifunga mwenyewe Dakika ya 21 na kisha Dakika ya 32 kuzua Penati baada ya kumchezea Rafu Abel Hernandez ambae alifunga Penati hiyo.
Hadi Mapumziko, Hull City 2 Man City 2.
Man City walifunga Bao la 3 Mfungaji akiwa Edin Dzeko kwenye Dakika ya 68 alipopewa Mpira na David Silva.
Frank Lampard, alietokea Benchi, aliipa Man City Bao la 4 katika Dakika ya 87 alipounganisha Krosi ya Pablo Zabaleta.
VIKOSI:
HULL CITY: McGregor, Dawson, Robertson, Rosenior, Davies, Huddlestone, Elmohamady, Diamé, Livermore, Hernández, Jelavic
Akiba: Bruce, Chester, Brady, Harper, Ramírez, Quinn, Ben Arfa
MAN CITY: Caballero, Zabaleta, Mangala, Clichy, Kompany, Silva, Fernandinho, Y Touré, Milner, Agüero, Dzeko
Akiba: Hart, Sagna, Kolarov, Jesús Navas, Lampard, Demichelis, Pozo
REFA: Anthony Taylor
SOUTHAMPTON 2 QPR 1
Southampton wameichapa QPR Bao 2-1 katika Mechi ya Ligi waliyocheza Nyumabini kwao.
Bao za Southampton zilifungwa na Ryan Bertrand na Graziano Pelle na lile la QPR kufungwa na Charlie Austin.
VIKOSI:
SOUTHAMPTON: Mignolet
Akiba:
QPR: Howard,
Akiba:
REFA: Mark Clattenburg
SUNDERLAND 0 SWANSEA 0
Stadium of Light hii Leo haikushuhudia hata Bao moja ila ilishuhudia Angel Rangel wa Swansea alipewa Kadi Nyekundu kwenye Dakika ya 81 baada ya kuzoa Kadi za Njano mbili.
Hadi mwisho Sunderland 0 Swansea 0.
VIKOSI:
SUNDERLAND: Mannone, Jones, van Aanholt, Vergini, O’Shea, Larsson, Rodwell, Cattermole, Johnson, Buckley, Wickham
Akiba:
SWANSEA CITY: Fabianski, Rangel, Fernandez, Williams, Taylor, Ki, Shelvey, Sigurdsson, Dyer, Routledge, Gomis
Akiba: Tremmel, Richards, Bartley, Montero, Carroll, Emnes, Bony
REFA: Chris Foy
0 comments Blogger 0 Facebook
Chapisha Maoni
Click to see the code!
To insert emoticon you must added at least one space before the code.