
Jumapili Januari 18
West Ham 3 Hull City 0
Man City 0 Arsenal 2
BAADA ya Miaka Mitano ya kubamizwa huko Manchester Leo hii Arsenal wametoka kidedea baada ya kuwacharaza Mabingwa wa England Manchester City 2-0 Uwanjani Etihad Jijini Manchester na wao kujiletea matumaini ya kufuzu 4 Bora huku wakiwaacha City wakiwa Pointi 5 nyuma ya Vinara Chelsea kwenye Msimamo wa Ligi Kuu England.
Ushindi huu umewafanya Arsenal wawe Nafasi ya 5 wakiwa Pointi 1 nyuma ya Man United walio Nafasi ya 4, Pointi 3 nyuma ya Timu ya 3 Southampton, Pointi 7 nyuma ya City na Pointi 12 nyuma ya Vinara Chelsea.
Kwa City hili ni pigo kubwa hasa baada ya kuwa na wimbi la Mechi 12 bila kufungwa na hasa ukizingatia Mechi yao inayofuata ya Ligi ni ya Ugenini hapo Januari 31 huko Stamford Bridge dhidi ya Chelsea.
Ushindi huu wa Arsenal ulianza kwa Penati laini aliyotoa Refa Mike Dean baada ya kuamua Vincent Kompany amemchezea Faulo Nacho Monreal na Santi Cazorla kufunga Penati hiyo katika Dakika ya 24.
Arsenal walifunga Bao lao la Pili Dakika ya 66 baada ya Frikiki ya Cazorla kuunganishwa kwa Kichwa na Olivier Giroud.

VIKOSI:
Man City: Hart; Zabaleta, Kompany, Demichelis, Clichy; Fernandinho, Fernando; Jesus Navas, Silva, Milner; Aguero
Akiba: Sagna, Dzeko, Kolarov, Caballero, Lampard, Mangala, Jovetic.
Arsenal: Ospina; Bellerin, Mertesacker, Koscielny, Monreal; Ramsey, Coquelin, Cazorla; Oxlade-Chamberlain, Giroud, Sanchez
Akiba: Szczesny, Gibbs, Rosicky, Ozil, Walcott, Flamini, Chambers.
REFA: Mike Dean














0 comments Blogger 0 Facebook
Chapisha Maoni