LOGO

Sterling runs off to celebrate his first goal of the night as Liverpool secured their place in the Capital One Cup semi-finalsMara baada mechi za Robo Fainal kukamilika katika Kombe la Ligi, Capital One Cup, ilifanyika Droo ya Mechi za Nusu Fainali na kushusha Bigi Mechi kati ya Liverpool na Chelsea.
Nusu Fainali nyingine itakuwa kati ya Tottenham na Sheffield United.
Mechi za Nusu Fainali zitachezwa kwa mikondo miwili ya Nyumbani na Ugenini kwenye Wiki inayoanzia Januari 19 na Marudiano yakiwa Wiki moja baadae.
Mapema Usiku huu wa Jumatano kabla Droo hii ya Nusu Fainali, Liverpool, wakicheza Ugenini kwa Vinara wa Timu ya Daraja la chini la Championship Bournemouth, walishinda Bao 3-1 kwa Bao 2 za Raheem Sterling na moja la Lazar Markovic  wakati Wenyeji hao walipata Bao lao pekee kupitia Dan Gosling.
Kwenye Mechi nyingine ya Robo Fainali iliyochezwa pia Usiku huu huko White Hart Lane, Tottenham waliitandika Newcastle Bao 4-0 kwa Bao za Bentaleb, Chadli, Kane na Soldado.
Jumanne Usiku, kwenye Robo Fainali za awali, Chelsea na Sheffield United zilishinda Mechi zao kwa Chelsea kuichapa Derby County 4-1 na Sheffield kuifunga Southampton 1-0.

0 comments Blogger 0 Facebook

Chapisha Maoni

ZILIZOSOMWA SANA

 
TASWIRA MICHEZONI © 2015. All Rights Reserved. This Blog Proudly Designed by MMC™ Media Group Ltd | Phone +255-786-758-021
Top