
Yapo Makundi Manne ya Timu 4 kila mmoja na Timu mbiliza juu toka kila Kundi zitaingia Robo Fainali.
Mechi za Makundi zitachezwa katika Miji ya Bata, Malabo, Mongomo na Ebebitin.
VIWANJA:
-Estadio de Bata, Mjini Bata, Watazamaji 37,500
-Nuevo Estadio de Malabo, Malabo, Watazamaji 15,250
-Estadio de Mongomo, Mongomo, Watazamaji 10,000
-Nuevo Estadio de EbebiyĆn, Ebebitin, Watazamaji 5,000
Leo zipo Mechi mbili za ufunguzi za Kundi A na ya kwanza ni ya Wenyeji Equatorial Guinea watakapocheza na Congo ndani ya Estadio de Bata Mjini Bata na kufuatia Mechi ya Burkina Faso na Gabon Uwanjani hapo hapo.
Kila Siku kutakuwa na Mechi mbili na Fainali ya Mashindano haya itachezwa Februari 8, Estadio de Bata, Mjini Bata.
Awali Mashindano haya yalikuwa yachezwe Nchini Morocco lakini Nchi hiyo ilijitoa kwa kuhofia Ugonjwa wa Ebola uliolipuka huko Afrika Magharibi na CAF kuipa Uenyeji Equatorial Guinea Nchi ambayo Mwaka 2012 iliweza pia kuwa Mwenyeji wa Mashindano haya pamoja na Gabon ambapo Zambia waliibuka Mabingwa.
0 comments Blogger 0 Facebook
Chapisha Maoni