LOGO



 
Wiki endi hii siku ya jumapili dunia itashuhudia mtanange mkali wa kukata na shoka kutoka kwa timu zinazoaminika kuwa na ushindani au upinzani mkubwa nchini England kutokana na historia zao mchezo huo utachezwa majira saa 10:30 kwa saa za Kitanzania..
Timu hizi zinapokutana shuhuli nyingine husimama kupisha mtanange huu mkubwa duniani ambao umeshasababisha vifo vya Mashabiki wengi tu wa Clabu hizi Maarufu duniani na Nchini England.
Manchester United inayofundishwa na Mdachi Louis van Gaal inaikaribisha Liverpoolinayofundishwa na Brendan Rodgers huku ikiwa na muenendo mzuri kwenye ligi ambapo wameshinda mechi 5 mfululizo huku Liverpool ikiwa na muenendo usioridhisha baada ya kutoka sare ya bila ya kufungana na Sunderland katika mchezo wa ligi ulioisha.
Mancheseter United ipo nafasi ya 3 kwenye msimamo wa ligi kuu nchini England EPL mara baada ya kuifunga Southampton huku vijogoo wa Liverpool wakiwa nafasi ya 9 huku katikati ya wiki hii wakiondoshwa nje ya michuano ya Uefa Champions League na timu ya FC Basel ya Uswisi.
Katika mchezo wa mwisho wa timu hizi kukutana kule nchini Marekani katika mechi za Pre Season Manchester United ilishinda jumla ya magoli 3 kwa 1 lakini mara yamwisho kukutana kwenye Ligi kuu Manchester United iliambulia kipigo kikali kutoka kwa Liverpool cha jumla ya Magoli 3-0 huku Man united ikiwa chini ya David Moyes mchezo huo ulifanyika kwenye dimba la Old Traford ambapo mwamuz Mark Clatenburg aliechezesha mchezo huo aliwazawadia Liverpool penalt 3 huku Nahodha Steven Gerrard akifunga mbili na Luis Suarez akifunga goli 1.
Kuelekea Mchezo huo Manchester United inaingia dimbani ikiwa na Majeruhi kibao ambapo Angel Di Maria bado atakosekana kweye mchezo huo kutokana na tatizo la Hamstring huku Chris Smalling akikiosekana pia baada ya kuumia kwenye mchezo ulipita huku Liverpool ikiendelea kumkosa Mshambuliaji wake Mahiri Daniel Sturidge na Rickie Lambart huku beki Kolo Toure akirejea dimbani ambapo alicheza mchezo wa katikati ya wiki dhidi ya FC Basel.
Timu hizo ambazo bado zinamatatizo ya Defensi zitaingia uwanjani huku zitigemea mbinu za makoxha zaidi katika kuamua mshindi wa mchezo huo au uwezo binafsi wa wachezaji wao nyota kama Robin van Persie, Wayne Rooney, Raheem Sterling na Felipe Coutinho.
Kocha Manchester United amewaonya wachezaji maarufu wa zamani timu hiyo kuwaache kuiongelea vibaya timu hiyo kwani hawajui kinachoendelea klabuni hapo hiyo imetokana Garry Nevile na Paul Scholes kuanza kuiongelea vibaya timu hiyo na kusema inacheza kama bata au mbwa haieleweki.

MCHI 5 ZA MWISHO KUKUTANA
·  United 0-3 L'pool (PL, Mar 14)
·  United 1-0 L'pool (LC, Sep 25)
·  L'pool 1-0 United (PL, Sep 13)
·  United 2-1 L'pool (PL, Jan 13)
·  L'pool 1-2 United (PL, Sep 12)

TIMU ZILIVYOKUTANA




MANCHESTER UNITED IMESHINDA 75
LIVERPOOL IMESHINDA MARA 64
SARE NI MECHI 51

TAKWIMU ZA WACHEZAJI
Steven Gerrard ndio mchezaji aliefunga magoli mechi Old Trafford magoli 5
Robin van Persie amefunga magoli 6 katika mechi 9 za mwisho dhidi ya Liverpool
Juan Mata amefunga magoli 4 katika Mashuti 5 yaliyolenga goli shots on target





0 comments Blogger 0 Facebook

Chapisha Maoni

ZILIZOSOMWA SANA

 
TASWIRA MICHEZONI © 2015. All Rights Reserved. This Blog Proudly Designed by MMC™ Media Group Ltd | Phone +255-786-758-021
Top