LOGO

Ligi daraja la kwanza Tanzania Bara (FDL) inatarajiwa kuanza kutimua vumbi siku ya Jumamosi, Oktoba 11 mwaka huu, ambapo timu 24 zitapambana kuwania nafasi tatu za kupanda Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara msimu wa 2015/2016.
Timu hizo zitakazoshiriki ligi hiyo zimegawanywa katika makundi mawili ya timu kumi na mbili kwa kila kundi. Mfumo utakaotumika ni ule wa kila klabu kucheza mechi za nyumbani na ugenini.
Kundi A linajumuisha timu za Lipuli,Tessema United, African Lyon, Friends Rangers, Villa Squad, Polisi Dar es Salaam, Majimaji, Ashanti United, JKT Mlale, Kimondo, Kurugenzi na African Sports.
Kundi B linazijumuisha timu za Toto African, JKT Kanembwa, Polisi Mara, Polisi Tabora, Mwadui,Mkamba Rangers, Burkina Faso, Green Warriors, JKT Oljoro, Rhino Rangers, Panone na Geita.

0 comments Blogger 0 Facebook

Chapisha Maoni

ZILIZOSOMWA SANA

 
TASWIRA MICHEZONI © 2015. All Rights Reserved. This Blog Proudly Designed by MMC™ Media Group Ltd | Phone +255-786-758-021
Top