LOGO

Mchezaji wa Simba FC inayoshiriki Ligi Kuu Uganda, Fahad Musana amefariki dunia ghafla wakati akiwa kwenye banda la video kushuhudia mechi ya Ligi Kuu England kati ya Manchester City na Chelsea juzi.
Kwa mujibu wa mtandao wa kawowo.com, Musana (24), alianguka sekunde chache tu baada ya Frank Lampard kuifungia Man City bao la kusawazisha katika mechi hiyo iliyomalizika kwa sare ya bao 1-1. Musana ni shabiki mnazi wa Chelsea. Kilichoshtua ni kwamba Musana alicheza mechi ya ligi dhidi ya Entebbe kwenye Uwanja wa Nakivubo Jumamosi iliyopita na timu yake iliibuka na ushindi wa bao 1-0.
Imeelezwa kwamba juzi Musana alifanya mazoezi na wenzake na kupata nao mlo wa mchana kabla ya kwenda kutazama mechi ya Manchester United na Leicester City kwenye banda hilo lililopo Bombo Mjini na baadaye akasubiri pia mechi ya klabu yake ya Chelsea. Musana alionekana kuwa na furaha wakati Chelsea ilipokuwa mbele kwa bao la Andre Schurrle, lakini baada ya Lampard kusawazisha tu alianguka na kufariki dunia. Maiti yake ilipelekwa katika Hospitali ya jeshi ya Bombo.
Fahad Musana
Tarehe ya kuzaliwa12 october 1990
iganga, Uganda
Tarehe aliyofariki21 de septiembre de 2014
(23 años)
LugaziUganda
TaifaBandera de Uganda Uganda
Nafasi anayochezaBeki/Defender
Alijiunga na Simba2010
Clabu anayochezeaSimba FC
Hadi mwaka2014
Alifariki akiwa mchezaji waSimba FC

0 comments Blogger 0 Facebook

Chapisha Maoni

ZILIZOSOMWA SANA

 
TASWIRA MICHEZONI © 2015. All Rights Reserved. This Blog Proudly Designed by MMC™ Media Group Ltd | Phone +255-786-758-021
Top