LOGO

Messi v Ronaldo
JUMAMOSI ndio Siku ambayo Vigogo wa Soka huko Spain, Real Madrid na FC Barcelona, watakapocheza Mechi yao ya kwanza ya La Liga Msimu huu Uwanjani Santiago Bernabeu kwenye pambano ambalo hubatizwa Jina rasmi ‘El Clasico.’
DONDOO MUHIMU:
-MFUNGAJI BORA DHIDI YA KIPA BORA: RONALDO v BRAVO!!
Msimu huu, Cristiano Ronaldo ameshapiga Bao 15 katika Mechi 7 za La Liga na anakutana na Kipa wa Barcelona Claudio Bravo ambae hajafungwa hata Bao 1 katika Mechi 7 za La Liga.
RONALDO ATAMTOBOA BRAVO?
-LUIS SUAREZ: KUCHEZA!
Meneja wa Barcelona, Luis Enrique, ametoboa kuwa Luis Suarez atacheza Mechi yake ya kwanza ya La Liga baada ya kumaliza Kifungo chake cha Miezi Minne lakini Meneja huyo amekataa kusema kama Straika huyo wa Urguay ataanza Mechi hiyo.
Safari hii, licha ya kuwapambanisha wale Masupastaa bora Duniani, Cristano Ronaldo, ambae ndiie rasmi Mchezaji Bora Duniani, na Lionel Messi, pia atakuwepo Mfungaji Bora Duniani, James Rodriguez, alietwaa Buti ya Dhahabu ya Fainali za Kombe la Dunia huko Brazil, akiichezea Real Madrid katika El Clasico yake ya kwanza.
Kivutio kingine, akicheza El Clasico yake ya kwanza, ni Straika mpya wa Barcelona, Luis Suarez, ambae hii huenda ikawa ni Mechi yake ya kwanza rasmi kuichezea Barca baada ya kumaliza Kifungo chake cha Miezi Minne alichopewa huko Brazil Mwezi Juni baada ya kumng’ata Beki wa Italy, Giorgio Chellieni, kwenye Mechi ya Fainali za Kombe la Dunia.
Pia Barca watatinga kwenye Mechi hii wakiwa chini ya Meneja mpya, Luis Enrique, alietwaa wadhifa mwishoni mwa Msimu uliopita baada ya kutimuliwa Gerardo Martino ambae aliiongoza Barca kumaliza Msimu uliopita wakiwa kapa bila Kombe lolote.
Uso kwa Uso
-Jumla Mechi: 227
-Real Madrid Ushindi: 91
-Sare: 48
-Barcelona Ushindi: 88
Real Madrid wao wamebaki na Meneja wao yule yule Mtaliana Carlo Ancelotti ambae Msimu uliopita aliiwezesha Real kutwaa Copa del Rey kwa kuifunga Barca 2-1 na pia kutwaa UEFA CHAMPIONZ LIGI baada ya kuwabonda Mabingwa wa Spain, Atletico Madrid, Bao 4-1 kwenye Fainali.
Jumamosi, Real watamkosa Mchezaji wao wa Bei ghali Duniani, Gareth Bale, ambae ameumia Musuli za Mguu zilizomfanya pia aikose Mechi ya Kundi lao la UEFA CHAMPIONZ LIGI waliyocheza Jumatano Usiku na kuichapa Liverpool 3-0 huko Anfield.
Kila Timu ina Wachezaji wapya ambao huenda wakacheza hii El Clasico na miongoni mwa hao ni pamoja na Jeremy Mathieu na Claudio Bravo wa Barca wakati Real wanae James Rodriguez na Toni Kroos.
Hadi sasa, baada ya Mechi 8, Barca wako kileleni mwa La Liga wakiwa na Pointi 8 na Real wapo Nafasi ya 3 wakiwa Pointi 4 nyuma yao huku Nafasi ya Pili ikishikwa na Sevilla wenye Pointi 19 wakati Mabingwa Watetezi Atletico Madrid wakiwa Nafasi ya 5 wakiwa na Pointi 17.
VIKOSI VINATARAJIWA:
Real Madrid: Casillas; Pepe, Sergio Ramos, Varane, Carvajal; Kroos, Modric, Rodriguez; Ronaldo, Benzema, Isco
Barcelona: Bravo; Pique, Alba, Alves, Mathieu; Mascherano, Iniesta, Xavi; Messi, Suarez, Neymar

MSIMAMO-Timu za Juu:
NA
TIMU
P
W
D
L
F
A
GD
PTS
1
FC Barcelona  
8
7
1
0
22
0
22
22
2
Sevilla FC
8
6
1
1
15
8
7
19
3
Real Madrid CF
8
6
0
2
30
9
21
18
4
Valencia
8
5
2
1
17
7
10
17
5
Atletico de Madrid
8
5
2
1
14
7
7
17

0 comments Blogger 0 Facebook

Chapisha Maoni

ZILIZOSOMWA SANA

 
TASWIRA MICHEZONI © 2015. All Rights Reserved. This Blog Proudly Designed by MMC™ Media Group Ltd | Phone +255-786-758-021
Top