LOGO

Ratiba ya ligi kuu ya Vodacom Tanzania bara (VPL) imetoka leo ambapo jumla ya timu 16 zinashiriki ligi hiyo itakayoanza kutimua vumbi Septemba 12 katika viwanja tofauti nchini na kumalizika Mei 7, 2016.
TFF inavisisitiza vilabu kukamilisha usajili wao wa wachezaji na viongozi kabla ya kufungwa kwa dirisha hilo la usjaili kesho siku ya Alhamisi Agosti 20, 2015. Baada ya kufungwa kwa usajili huo hakutakuwa na muda tena wa nyongeza.
Kwa klabu ambayo haitawasilisha malipo ya ada ya mchezaji wa kigeni ya dola elfu mbili (U$D 2000) mchezaji huyo hataruhusiwa kucheza kwenye ligi hadi malipo hayo yatakapofanyika. 
Michezo saba itachezwa siku ya ufunguzi Jumamosi Septemba 12 katika viwanja tofauti ambapo mechi zitakuwa kama ifuatavyao; Ndanda Vs Mgambo Shooting (Nang’wanda – Mtwara), African Sports Vs Simba SC (Mkwakwani – Tanga), Majimaji Vs JKT Ruvu (Majimaji – Songea), Azam FC Vs Tanzania Prisons (Azam Complex – Dsm), Stand United Vs Mtibwa Sugar (Kambarage – Shinyanga), Toto Africans Vs Mwadui (CCM Kirumba – Mwanza), na siku ya jumapili Young Africans Vs Coastal Union (Taifa – Dar es salaam).
Ratiba kamili hii hapa, angalia mechi zote za timu yako hapo chini…
Vodacom Premier_Page_1
Vodacom Premier_Page_2
Vodacom Premier_Page_3
Vodacom Premier_Page_4
Vodacom Premier_Page_5
Vodacom Premier_Page_6
Vodacom Premier_Page_7

0 comments Blogger 0 Facebook

Chapisha Maoni

ZILIZOSOMWA SANA

 
TASWIRA MICHEZONI © 2015. All Rights Reserved. This Blog Proudly Designed by MMC™ Media Group Ltd | Phone +255-786-758-021
Top