Hans alianza na Mrisho Ngassa, Andrey Coutinho, Simon Msuva, Hassan Dilunga na Salum Telela kwenye kiungo kitu kilichowawia vigumu vijana wa Jang'ombe kutawala mchezo huo.
Pamoja na mabao hayo ya Yanga, bado safu ya ulinzi hasa mabeki wa kati walionekana kufanya makosa mara kadhaa ambapo Nahodha Nadir Haroub alicheza na Pato Ngonyani na kama washambuliaji wa Jang'ombe wangekuwa makini, wangeweza kujipatia mabao hasa kipindi cha kwanza.
Matokeo hayo yanakamilisha idadi ya timu nne zinazoshiriki michuano hiyo kutoka Tanzania bara kukamilisha mzunguko wa kwanza wa makundi hayo huku Simba ikiwa ndiyo timu pekee ambayo haina alama hata moja baada ya hapo jana kufungwa bao 1-0 na Mtibwa Sugar huku Azam Fc kwenye mchezo wa mapema leo wakitoka sare ya bao 2-2 na KCCA ya Uganda.
0 comments Blogger 0 Facebook
Chapisha Maoni