Swansea ndio walitangulia kufunga Bao kupitia Straika wa Ivory Coast Wilfried Bony na West Ham kujibu mapigo kwa Bao 2 za Vichwa za Andy Carroll na moja la Diafra Sakho, Straika kutoka Senegal.
Dakika 2 tu baada ya kupigwa Bao la Pili, Swansea walibaki Mtu 10 baada ya Kipa wao Lukasz Fabianski kupewa Kadi Nyekund kwa kumchezea Rafu Diafra Sakho lakini Refa kwanza alipeta Faulo hiyo na kumwacha Sakho aende kufunga lakini alikosa baada ya kupiga Posti na Refa Chris Foy kuamua kumtoa Kipa huyo wa zamani wa Arsenal.
MAGOLI:
West Ham 3
-Andy Carroll (41', 66')
-Diafra Sakho (87')
Swansea City 1
-Wilfried Bony (19')
Kadi Nyekundu
KADI NYEKUNDU
-Lukasz Fabianski (68')
West Ham sasa wana Pointi 27 kwa Mechi 15 wakiwa nyuma ya Man City yenye Pointi 33 na Vinara Chelsea wenye Poinyi 36 huku wakiwa mbele kwa Pointi 1 dhidi ya Southampton na Pointi 2 mbele ya Man United.
VIKOSI:
West Ham: Adrian, Jenkinson, Tomkins, Reid, Cresswell, Kouyate, Song, Downing, Nolan, Valencia, Carroll
Akiba: Zarate, Sakho, O’Brien, Collins, Amalfitano, Jaaskelainen, Cole. Swansea: Fabianski, Rangel, Bartley, Williams, Richards, Britton, Ki, Routledge, Sigurdsson, Montero, Bony
Akiba: Amat, Shelvey, Dyer, Carroll, Gomis, Tiendalli, Tremmel.
REFA: Chris Foy
Carroll rose majestically above the Swansea defence to send the ball looping towards the net and put his team in front
0 comments Blogger 0 Facebook
Chapisha Maoni
Click to see the code!
To insert emoticon you must added at least one space before the code.