Barcelona imemfukuza kazi Andoni Zubizarreta kutoka nafasi yake ya Mkurugenzi wa Soka.
Zubizarreta,
mwenye Miaka 53 na Kipa wa zamani wa Barcelona, alichukua wadhifa huo
wa Mkurugenzi mwanzoni mwa Msimu Mwaka 2010 baada ya kuondoka kwa Txiki
Begiristain ambae sasa yupo Manchester City kama Mkurugenzi wa Soka.
Taarifa ya Klabu ya Barcelona ilisema Rais wao Josep Maria Bartomeu ameamua kuvunja Mkataba na Zubizarreta mara moja.
Zubizarreta alikuwa Kipa wa Barca kati ya Miaka 1986 na 1994 na pia kuidakia Spain mara 126.
Huko
Spain Wadau wengi wamekuwa wakimlaumu Zubizarreta, ambae alihusika na
Uhamisho wa Wachezaji, kwa janga la kufungiwa na FIFA kuuza na kusajili
Wachezaji wapya kwa Mwaka huu wote kutokana na kukiuka Kanuni za
Kusajili Wachezaji Chipukizi wa chini ya Miaka 18 kutoka nje ya Spain.
0 comments Blogger 0 Facebook
Chapisha Maoni