Mchezo huo ulishuhudia kikosi cha Azam kikiwakosa Kipre Tchetche, Kipre Balou na Didier Kavumbangu ambao ni wagonjwa huku beki David Mwantika kwa mara ya kwanza akicheza sambamba na Agrey Morris kwenye safu ya ulinzi huku beki raia wa Ivory Coast, Pascal Wawa akianzia benchi.
Katika mchezo huo, kocha Joseph Omog alimtoa mapema kiungo Amri Kiemba kwenye mchezo huo huku KCCA nao wakimtoa Owen Kasule baada ya kuonekana kutokuwa kwenye ubora huku kiungo mshambuliaji mpya wa Azam, Brian Majwega akionyesha kiwango bora kabisa kwenye mchezo huo.
Michezo mingine ya timu kutoka bara ilichezwa jana pale Mtibwa Sugar walipocheza na Simba na kuwalaza bao 1-0 na muda mfupi ujao, timu ya Yanga itashuka dimbani kumenyana na Timu ya Taifa ya Jang'ombe huku mashabiki wa wana Jangwani hao wakiwa na matumaini makubwa na timu yao.
0 comments Blogger 0 Facebook
Chapisha Maoni
Click to see the code!
To insert emoticon you must added at least one space before the code.