Klabu ya Manchester City ya England ilibidi isubiri hadi mechi ya misho ya makundi ili kujua hatima yao hiyo imekuja baada ya kutoanza vizuri ligi hiyo ya mabingwa barani ulaya.
Ushindi dhidi ya AS Roma ya Italia katika uwanja wa Olympico uliipitisha timu hiyo ya Etihadi kupita katika hatua ya 16 bora kwa kuichapa jumla ya magoli 2-0 huku Man city ikimkosa Mshambuliaji mahiri Sergio Aguero kwa tatizo la majeruhi.
Man City walionekana kuwa na bahati au walichanga vizuri karata zao baada ya beki Pablo Zabaleta kuifungia Man City bao la pili katika dakika ya 87 na kuihakikishia City ushindi huo ugenini
Kwa ushindi huo City wamefikisha Point 8 na kushika nafasi ya Pili nyuma ya vinara Bayarn Munich wenye point 15 hivyo AS Roma watacheza Michuano ya Europa kwa kushika nafasi ya 3
0 comments Blogger 0 Facebook
Chapisha Maoni