Klabu ya Manchester united imeendeleza wimbi la ushindi katika michezo ya ligi kuu kwa kuichapa timu ngumu ya Southampton jumla ya magoli 2-1 katika mchezo uliochezwa kwenye uwanja wa St Marys majira ya saa 5 usiku kwa saa za Tanzania.
Ingawa Man united haikucheza katika kiwango kikubwa ila ilifanikiwa kudhibiti mashambulizi ya Southampton kwa muda wote wa mchezo huku beki Chris Smalling akipata majeraha na kutolewa na nafasi kuchukuliwa na Jonny Evans.
Mholanzi Robin Van Persie ndie alieipa uongozi Man united kwa kufunga goli la kwanza katika dakika ya 12 kufuatia makosa beki wa Southampton Jose Fonte na kufanya matokeo Southampton 1 Man united 1. Southampton walijaribu kusawazisha bila mafanikio lakini katika dakika ya 31 Mshambuliaji Graziano Pelle aliisawazishia Southampton na kufanya matokeo kusomeka 1-1 hadi mapumziko.
Katika kipindi cha pili Man united ilionekana kuzidiwa na wenyeji ambapo Southampton walikosa nafasi nyingi za wazi huku goli kipa wa Man united akiokoa michomo mingi golini kwake.
Katika dakika 71 Robin Van Persie tena anaihakikishia ushindi na point 3 muhimu timu yake ya Man united kwa kuifungia bao la pili na ushindi kufuatia mpira wa faulo uliopigwa na Wayne Rooney.
Soutampton walijaribu kurudisha bila Mafanikio na mpaka dakika 90 zinakamilika Man united ilmeibuka ushindi wa magoli 2-1 na ushindi unakuwa ni ushindi wa 5 mfululizo ukiwa weka hadi nafasi ya 3 huku Southampton wao wakipoteza mechi 3 mfululizo na kuambulia nafasi ya 5
VIKOSI
Southampton: Forster, Clyne, Fonte, Yoshida, Bertrand, Steven Davis, Wanyama, Long, Tadic, Mane, Pelle.
Subs: Kelvin Davis, Gardos, Mayuka, Isgrove, Reed, Targett, Hesketh.
Goal: Pelle 31
Man Utd: De Gea, McNair, Smalling, Rojo, Carrick, Valencia, Fellaini, Mata, Young, van Persie, Rooney.
Subs: Evans, Falcao, Januzaj, Lindegaard, Ander Herrera, Fletcher, Wilson.
Goals: Van Persie 12, 71
Referee: Kevin Friend (Leicestershire)
0 comments Blogger 0 Facebook
Chapisha Maoni